MASWALI YA MITIHANI KIDATO CHA NNE (SEHEMU "C")



SEHEMU C UANDISHI.
NECTA 2007-(CANDIDATE)
Qn5. Andika insha yenye maneno mia moja (100) kuhusu moja ya mada zifuatazo:-
(a)  Maandalizi ya uchguzi mkuu wa Oktoba 2005.
(b) Upimaji wa virusi vya ukimwi.
(c)  Mwenda tazi na omo marejeo ngamani.

NECTA 20080(BOTH)
Qn8. Muundo wa uandishi wa barua za kirafiki na barua za kikazi ni tofauti. Thibitsha kauli hiyo.
Qn9. Manyanda akiwa mfanyakazi wa kiwanda cha korosho Tanitaalipewa taarifa kuhusu ugonjwa wa baba  yake. Wewe kama Manyanda andika barua ya kuomba ruhusa.  Anuani ya kiwanda ni S.L.P. 1030, Kibaha.

NECTA 2009. (CANDIDATE)
Qn8. Andika insha  yenye maneno 250 kuhusu moja ya mada zifuatazo:-
(a)  Aisifiaye mvua imemnyeshea.
(b) Elimu ya msingi ina umuhimu wake katika jamii.
(c)  Maradhi yanavyorudisha nyuma maendeleo ya familia hatimaye Taifa.
(d) Kueleimika kwa msichana ni kueleimika kwa jamii.
(e)  Wanyama pori.
Qn9. Katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwako, unahitaji marafiki kwa ajili ya kusherehekea siku hiyo. Andaa kadi ya mwaliko ili kuwapa taarifa rafiki zako.

NECTA-2010 (CANDIDATE)
Qn8. Eleza tofauti iliyopo kati ya hotuba na risala. Andika hotuba kuhusu “Maji ni uhai.”
Qn9. Wewe kama afisa ununuzi, andika barua kwa mfanyabiashara mashuhuri wa wilayani kwenu kuhusu  agizo la bidhaa.

NECTA-2011 (CANDIDATE)
Qn8. Andika insha isiyo ya kisanaa yenye maneno mia mbili na hamsini 250 kuhusu mandhari ya shule yenu.
Qn9. Andika kumbukumbu za kikao cha wanafunzi kuhusu sherehe ya kumuaga mkuu wenu wa shule aliyepata wadhifawa kuwa Afisa elimu wa Mkoa.

NECTA-2012 (CANDIDATE)
Qn8. Jifanye kuwa umepata barua ya mwaliko wa sherehe ya siku ya kuzaliwa ya rafiki yako aitwaye Faraja Matata, itakayofanyika siku ya tarehe 10/10/2012. Kwa bahati mbaya siku tatu kabla ya sherehe umepatwa na safari ya kikazi kuelekea mkoani Singida. Andika barua ya kumtaarifu rafiki yako kuwa hutaweza kuhudhuria sherehe hiyo. Jina lako liwe Tumaini Baraka.
Qn9. Andika insha yenye maneno ysiyopungua mia mbili na hammsini (250) na yasiyozidimia tatu (300) kuhusu umuhimi wa huduma za simi ya mkononi.

NECTA-2013 (CANDIDATE)
Qn8. Wewe ni mfanya biashara mahsuhuri mjini Dodoma. Andika barua ya kutuma bidhaa kwa mteja wako aitwaye Dunia Msimbo anayeishi Lindi. Jina lako liwe Nyila Sasisha.
Qn9. Andika tangazo katika gazeti la Rai ukitoa taarifa kuhusu kupotea kwa mwanao aitwaye Raha Karaha, jina lako liwe Furaha Machupa.

NECTA-2013 (PRIVATE)
Qn8. Wewe ni Kiranja mkuu wa shule ya Sekondari Kazamoyo iliyoko Tanga, jina lako Uwezo Jitihada na unasoma kidato cha nne. Andika barua kwa mkuu wa Shule ukiomba ruhusa ya kuhudhuria semina ya uelimishaji rika itakayofanyika tarehe 10/11/2013 katika Shule ya Sekondari Tutafika iliyoko Moshi. Barua yako ipitie kwa Mwalimu wa darasa.
Qn9. Jifanye wewe una elimu ya kidato cha nne, jina lako Situmai Kasheshe unayeishi katika kijiji cha Songambele kilichopo wilayani Mpanda. Tumia taarifa zilizomo kwenye tangazo lifuatalo lililotolewa kwenye gazeti la Mwananchi tarehe 01/12/2013 kuandika barua ya maombi ya kazi.
TANGAZO LA NAFASI YA KAZI
KAZI: Karani Masijala
SIFA:
·         Awe amehitimu kidato cha nne na kufaulu masomo ya kiingereza na Hisabati
·         Awe na uri usiozidi miaka 35
·         Awe mtanzania
·         Awe na ujuzi wa kompyuta

Barua ya maombi iambatanishwe na nakala za vyeti na itufikie kala ya tarehe 15/12/2013.

Maombi yote yatumwe kwa:

Afisa Mwajiri
Kampuni ya Kutengeneza Masufuria
S.L.P 600
KATAVI





NECTA-2014 (BOTH)

Qn8. Andika insha yenye maneno yasiyopungua mia mbili (200) na yasiyozidi mia tatu (300) kuhusu methali isemayo “Samaki mkunje angali mbichi.”
Qn9. Wewe ni mwenyekiti wa mtaa abao umekumbwa na mafuriko lakini wananchi wako wanakataa kuhamia makazi mapya. Andika hotuba utakayoitoa kwa wananchi wa mtaa wako ili kuwashawishi kuondoka katika sehemu hiyo. Jina la mtaa ni Kwamachombo na eneo la makazi mapya linaitwa Kitivo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment